Unordered List

Pages

Tuesday, January 1, 2013

MWANAJESHI ALIYEPIGA PICHA NA LEMA ATOROKA

>>> JESHI LAENDELEA KUMSAKA JESHI la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), limesema askari anayedaiwa kuwa jeshi hilo aliyepiga picha na Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema ametoroka. Msemaji wa JWTZ, Kanali Kapambala Mgawe alisema jana kwamba pamoja na hatua yake ya kutoroka, jeshi litaendelea kumsaka kwa udi na uvumba ili kumhoji na kujiridhisha kama kweli ni mwanajeshi wake kabla ya kumchukulia hatua za kinidhamu kwa mujibu wa Kifungu cha 147 cha Katiba ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania ya 1977. “Huyu kijana inasemekana alishawahi kupitia Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), lakini wakati tunaendelea...

Saturday, December 29, 2012

MNYIKA-TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Nakusudia kutumia kifungu cha 10 cha Sheria ya ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge kutaka nakala ya mkataba wa mkopo wa masharti kiasi cha Dola za Marekani bilioni 1.225 (shilingi trilioni 1.86) kutoka China. Nitataka pia nakala za mikataba wa mradi wa miundombinu ya gesi asilia ambayo itahusisha ujenzi wa mitambo ya kusafishia gesi asilia katika mikoa ya Lindi na Mtwara na ujenzi wa bomba kuu la kusafirishia gesi asilia la inchi 36 kutoka Mtwara kupitia Lindi, Pwani hadi Dar es Salaam lenye umbali wa kilometa 532. Hii ni kwa sababu mpaka sasa Wizara ya Nishati na Madini haijatekeleza pendekezo nililowasilisha bungeni tarehe 27 Julai 2012 kwamba kutokana na unyeti wa mradi huo kwa mustakabali wa nchi na maisha ya wananchi wa sasa na baadaye Serikali ilipaswa kuwasilisha bungeni...

Wednesday, November 28, 2012

Wabunge wa Kigoma wamtunishia misuli RC

Wabunge wa Mkoa wa Kigoma wamemtunishia misuli Mkuu wa Mkoa huo, Kanali Mstaafu Issa Machibya, kutokana na kuwatishia kuwafunga pingu kama raia wengine wa kawaida, wakisema kauli hiyo ni dharau kubwa kwao wakiwa ni moja ya mihimili mitatu ya dola wenye jukumu la kuishauri na kuisimamia serikali, hivyo anapaswa kuwaomba radhi. Kanali Machibya anadaiwa kutoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki iliyopita mbele ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, katika kongamano la uwekezaji Kanda ya Ziwa Tanganyika, mkoani Katavi, kwa kutamka kwamba, mbunge yeyote atakayekaidi maelekezo yake au maelekezo ya mkuu wa wilaya atakamatwa na kupigwa pingu kama raia wengine wa kawaida. Wakuu wa mikoa mitatu inayounda ukanda huo, ambayo ni Kigoma, Katavi na Rukwa, walihudhuria kongamano hilo pamoja na...

Thursday, November 22, 2012

SEHEMU YA PILI: Mahojiano ya moja kwa moja na Mhe. Zitto Zuberi Kabwe katika JamiiForums

MHOJAJI: Mkuu Zitto nashukuru kwa majibu yako kina kwa swali la kwanza, swali linalofuata; B. Zitto na CHADEMA 1) Nini kipaumbele chako cha sasa kama mwanachama wa CHADEMA? 2) Mkuu, ni kweli kuwa CHADEMA ni chama cha kidini/kikabila? Na kama ni kweli, tatizo hilo lishughulikiwe vipi? Kama si kweli, unaweza kuueleza umma wa watanzania una kauli gani juu ya mitizamo hii dhidi ya chama chenu? 3) Mh. Zitto, unaizungumziaje demokrasia ndani ya chama chako katika chaguzi, teuzi na kupanga safu za uongozi? 4) Kwanini CHADEMA haiwatumii viongozi wa Mikoa na Wilaya na badala yake inatuma watu toka makao makuu hata kwa mambo madogo madogo ambayo yangemalizwa na uongozi wa ngazi husika? 5) ...

Wednesday, November 21, 2012

KAMA HUKUPATA NAFASI YA KUSOMA MAHOJIANO YA ZITTO KWENYE JAMII FORUM NAKULETEA MAHOJIANO YA AWALI

>>MASWALI NA MAJIBU YA ZITTO KABWE NA JF  ZITTO:Re: Mahojiano ya moja kwa moja na Mhe. Zitto Zuberi Kabwe katika JamiiForums Awali ya yote itoe shukrani zangu za dhati kwa kupewa fursa hii adimu ya kuhojiwa na wana JF wenzangu. Nashukuru pia kwa kuwa ni heshima kubwa sana kwangu maana mimi ni mtu wa pili kufanyiwa mahojiano kama haya baada ya kijana mwenzetu Maxence kama 'founder' wa jukwaa letu. Napenda pia ifahamike kuwa mimi ni mmoja wa wanachama waanzilishi wa jukwaa hili na ninafurahi kuona limekuwa na kwa kweli its a force to reckon with. Zitto ni Mtanzania aliyezaliwa Kigoma, Kijiji cha Mwandiga. Nimekulia katika kitongoji cha Mwanga, nimekwenda shule ya Msingi Kigoma, Sekondari Kigoma, Kibohehe Moshi, Galanos Tanga na Tosamaganga Iringa. Nimepata...

MAHOJIANO YA ZITTO KABWE LIVE MUDA HUU JAMII FORUM

Mahojiano ya moja kwa moja yameanza katika thread hii - Mahojiano ya moja kwa moja na Mhe. Zitto Zuberi Kabwe katika JamiiForums Na hivyo mnakaribishwa kufuatilia, thread hii ni kwa ajili ya side comments na ile ya mahojiano itaendeshwa na AshaDii na atakuwa anajibizana na Mhe. Zitto. FUATILIA MAHOJIANO HAYO HAPA KWA KUBONYEZA LINK HII>>>>>>>>>>>>>>>>>>  ...

Monday, November 19, 2012

J.K ni Jembe. ## MAKALA FUPI KUTOKA KWA MJENGA WA "JF"

Haina ubishi kuwa J. Kikwete ni rais pekee ametawala kwa mizengwe lakini namna anavyoipangua mizengwe hiyo, anastahili pongezi kubwa. Ikumbukwe zengwe la kwanza ni lile la kukataliwa na CHADEMA kuwa si rais halali, wakaenda mbali zaidi kwa wabunge wake kumzilia hotuba yake ya ufunguzi na kutoka nje ili kumdhalilisha, huku katibu mkuu kutangaza kuwa atahakikisha J.K hatawali. Kikwete kwa umahiri mkubwa alitulia na kuendelea kuhutubia huku akiwahakikishia kuwa "ipo siku watarudi kwake" (walirudi hawakurudi?). Zengwe lingine ni la kudai kumshtaki J.K kwa wananchi ili kumshinikiza aondoke madarakani. Hili pia lilifanywa na CHADEMA kupitia maandamano sehemu mbalimbali za nchi wakilenga zaidi kutengeneza propaganda ya kuidanganya jumuiya ya kimataifa kuwa J.K hakubaliki na wananchi. Hilo...

Pages 51234 »
Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More

 
Powered by Blogger