Unordered List

Pages

Friday, September 28, 2012

CCM YASHINDA UMEYA JIJI LA MWANZA

UFAFANUZI KILICHOTOKEA KWENYE UCHAGUZI WA UMEYA WA JIJI LA MWANZA KATI YA CCM NA CHADEMA.

Mgombea wa kiti cha umeya katika Halmashauri ya jiji la Mwanza kupitia CCM na diwani wa kata ya Mkolani Ndg Stanslaus Mabula, ameshinda kiti cha Umeya wa Halmashauri ya Nyamagana kwa jumla ya kura 11 dhidi ya mgombea wa CHADEMA diwani wa kata ya Mahina Ndg Charles Chibara aliyepata kura 8.

CCM wameshindishwa na mbinu za kisiasa amabzo uhalali wake kisheria linabaki kuwa suala la wanasheria wanaojua taratibu zikoje kutufafanulia.

Baada ya mgawanyo wa Halmashauri ya jiji la Mwanza na kuwa na halmashauri ya jiji inayoundwa na Majimbo mawili, kulipatikana Halmashauri ya Nyamagana inayoundwa na Jimbo la Nyamagana na halmashauri ya ilemela inayondwa na jimbo la Ilemela.

Mgawanyo huo ulifanyika Mwezi Julai mwaka huu ambapo Mgawanyo wa Madiwani ukabaki ifuatavyo;

NYAMAGANA.

CHADEMA - MADIWANI WA KUCHAGULIWA - 5, MADIWANI WA VITI MAALUM - 2, MBUNGE - 1. JUMLA CHADEMA WANAKUWA NA WAJUMBE 8 WA BARAZA LA MADIWANI WA HALMASHAURI YA NYAMAGANA.

CCM - MADIWANI WA KUCHAGULIWA - 6, MADIWANI WA VITI MAALUM - 1, MBUNGE - 0. JUMLA CCM WANAKUWA NA WAJUMBE 7 WA BARAZA LA MADIWANI WA HALMASHAURI YA NYAMAGANA.

CUF - DIWANI WA KUCHAGULIWA -1, DIWANI VITI MAALUM -1, MBUNGE 0. JUMLA WANAKUWA NA WAJUMBE WAWILI WA BARAZA LA MADIWANI LA HALMASHAURI YA NYAMAGANA.

ILEMELA.

CHADEMA - MADIWANI WA KUCHAGULIWA - 6, MADIWANI WA VITI MAALUM - 2, MBUNGE - 1. JUMLA CHADEMA WANAKUWA NA WAJUMBE 9 WA BARAZA LA MADIWANI WA HALMASHAURI YA ILEMELA.

CCM - MADIWANI WA KUCHAGULIWA - 3, MADIWANI WA VITI MAALUM - 2, MBUNGE - 1. JUMLA CCM WANAKUWA NA WAJUMBE 6 WA BARAZA LA MADIWANI WA HALMASHAURI YA ILEMELA.

CUF - DIWANI WA KUCHAGULIWA - 0, DIWANI VITI MAALUM - 0, MBUNGE 1. JUMLA WANAKUWA NA WAJUMBE WAWILI WA BARAZA LA MADIWANI LA HALMASHAURI YA ILEMELA.

SIASA NI MIPANGO - MBINU ZA CCM HALMASHAURI YA NYAMAGANA.

Kilichotokea ni CCM kuhamisha Diwani Mmoja wa Viti Maalum na Mbunge Mmoja wa viti maalum (kwa barua yao kwenda ya tarehe 14, Septemba, 2012 kwa mkurugenzi wa Jiji) kutoka Halmashauri ya Ilemela kuja Halmashauri ya Nyamagana na hivyo kuongeza idadi ya kura zao kuwa 9.

Wakati huo huo Chadema walishakuwa hawaihehabu kura ya Diwani wao wa Kata ya Igoma Bwana Chagulani Adams ambaye wamemfukuza/wamemvua Uanachama na amerejeshwa na mahakama Barazani wakati akisubiri kusikilizwa kwa kesi yake aliyoifungua kupinga kuvuliwa Uanachama, Hivyo kuwafanya Chadema wao wapungukiwe na Mjumbe Mmoja na hivyo kubaki na Wajumbe 7 .

Matokeo mara baada ya Kura kupigwa ni kuwa CCM walipata kura 11 na Chadema walipata Kura 8 na hivyo CCM kuwa Washindi wa Kiti cha Umeya wa Halmashauri ya Nyamagana.

HISIA/DHANA.

Kulingana na Tathmini hiyo hapo juu kumezuka dhana na hisia kuwa Kura zilipigwa ifuatavyo:

CCM: Walipata kura zote za Wajumbe wao 9 NA PIA WAKAPATA NYONGEZA YA KURA 2 ZA WAJUMBE WA CHADEMA.
CCM: Walipata kura zote za Wajumbe wao 9 NA PIA WAKAPATA NYONGEZA YA KURA 2 ZA WAJUMBE WA CUF.
CCM: Walipata kura zote za Wajumbe wao 9 NA PIA WAKAPATA NYONGEZA YA KURA 2 ZA MJUMBE MMOJA WA CHADEMA NA MJUMBE MMOJA WA CUF.

MUAFAKA WA CHADEMA B/CCM B (CUF) NA CHADEMA.

Pamoja na kuitwa CCM B kwa kuwa na MUAFAKA na CCM kule Zanzibar Lakini pia CUF walipata jina jipya la CHADEMA B kwa kuwa na Muafaka na Chadema ambapo walikubaliana kuungana mkono katika Uchaguzi huo.

Kamati ya utendaji ya Chadema Nyamagana, kushirikiana na kamati za madiwani wa Chadema zilikamilisha mchakato wa kupata Mgombeawa nafasi ya Umeya mara baada ya Diwani wa Kata ya Maina, Charles Chibara, kupitishwa kuwa mgombea Umeya wa Halamashauri Hiyo.

Chadema walifanya makubaliano na chama cha CUF ili wapate wingi wa kura na kumpitisha Diwani wa CUF Kata ya Mirongo Daudi Mkama, kuwa mgombea wa nafasi ya Naibu Meya.

CUF wanadai walitekeleza Makubaliano yao na Chadema na hivyo kura zao zote 2 waliipigia Chadema na hivyo kuonyesha kuwa Chadema walipata Kura 7 kutoka kwa Wajumbe wake Halali (Ukimuondoa "Diwani wa Mahakama" Chagulani Adams).

Ni vigumu kuthibitisha Uhalali wa Madai ya Cuf kupiga Kura zao 2 kwa Chadema kama ambavyo ni vigumu kuthibitisha Kinyume chake, AKILI KUMKICHWA.

MWARI ALALA ILEMELA.

Hayo yakiendelea uchaguzi wa Meya wa Ilemela umeahirshwa katika mazingira tata, baada ya Mkurugeni kusoma Amri ya Mahakama iliyopewa tafsiri na Mwanasheria wa jiji kuwa inakifanya kikao hicho kuahirishwa kwa kuwa "Diwani wa Chadema wa Mahakama" wa Kata ya Kitangiri Bwana Matata (ambaye naye pia alifukuzwa/alivuliwa Uanachama pamoja na yule Diwani wa Igoma na anaendelea na Udiwani kwa Amri ya Makahama) kuleta Barua ya kutaka atambuliwe kama Mgombea.

Ukazuka ubishi kidogo juu ya hoja ya Mgombea kuteuliwa na chama, Mkurugenzi wa Jiji akasema hiyo siyo sheria ni mwogozo, na kwa kuwa sheria na mwongozo zikigongana sheria ndiyo inatamalaki hataki aingie katka Mgogoro wa Tafsiri ya Sheria, Hivyo akaamua kuaghirisha Kikao.

HOJA YA KISHERIA YA CHADEMA.

Kwa mujibu wa mwanasheria wa wa Chadema, pingamizi hilo la Mahakama juu ya Chadema kumvua Uanachama Diwani Matata lilikuwa linamrejeshea Diwani huyo haki yake ya Uanachama na hivyo kuendelea na Udiwani wake, na kutaka matata asizuiliwe kuendelea na mchakato wa kuomba Umeya.

Mwanasheria huyo aliendelea kusema kuwa kwa mantiki hiyo Matata ameomba uteuzi wa Chama lakini hakuteuliwa na Chama na hivyo Mahakama haiwezi kuwalazmisha chama wateue mgombea kwa Amri ya Mahakama. Yeye anaamini ni uhuni tu na njama za kisiasa zimefanyika kuaghirisha uchaguzi huo.

USHAURI HURU WA KISHERIA.

Bado nawasiliana na Wanasheria Mbalimbali ili kupata Ushauri huru wa Kisheria juu ya Suala hili.

HONGERA WASHINDI, ASHINDWAE PIA NI MUME.

Nichukue Fursa hii kuwapongeza CCM KWA uSHINDI WAO, Hongereni sana. Poleni sana Chadema na pia Poleni sana CCM B/CHADEMA B (CUF).

ABALHASSAN.

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More

 
Powered by Blogger