WAKUU WANA-JF

Kwa kipindi kisicho zidi muda wa miezi mitatu(3) kumekuwa na lugha ama sentesi kadhaa kutoka kwa Mh. Freeman Mbowe ambaye ni mwenyekiti wa CHADEMA taifa ambazo wachambuzi wa kisiasa kama sisi ni lazima tuzijadili kwa kina kwa sababu hatujawahi kuzisikia kutoka kinywani kwa Kiongozi huyu siku za nyuma pia ni haba sana kuzisikia hasa kwa CHAMA MAKINI KAMA CHADEMA katika taifa hili.

Mbowe akiwa kama nguzo imara ya upinzani na amekuwa na machngo mkubwa sana katika harakati za ukombozi ndani ya taifa hili,Lakini lugha zake za hivi karibuni zina ukakasi mkubwa sana pia ni tata kwa wananchi ambao wanaamini kabisa CHADEMA kinaweza kuwa chama mtambuka cha ukombozi ndani ya taifa hili.

KAULI TATA AMBAZO ZINAZUA MASWALI MENGI KUTOKA KWA MH:FREEMAN AIKAEL MBOWE NI HIZI
1. Kupitia gazeti la majira la wiki tatzu zilizopita Mh.Freeman mbowe alinukuliwa akisema Yupo tayari kuachana na chadema wakati wowote atakapo amua.

Kauli hii ni tata na mlengo wake unazua maswali mwengi sana.Tujiulize mbowe anasema kuwa anatakuacha na siasa za CHADEMA wakati wotete Je ni kwamba amechoka kupigana na CCM?Au ameshavuna mazao ya siasa na hahitaji tena kuendelea kuyala?Naweza kwenda mbali kabisa kwamba Mbowe anapotangaza kuachana na siasa za CHADEMA ni kwamba anataka kuudhihirishia umma kuwa CHADEMA si mali yake(familia) kama wengi wanavyokitafsili?

Lakini kauli kama hii mbowe haoni kama anakatisha tamaa kwa viajana ambao wamekuwa wakijiunga na CHADEMA kutokana na yeye kuwa mwanaharakati makini kwa muda mrefu?

2. Kupitia GAZETI LA TANZANIA DAIMA wiki iliyopita Mh.Mbowe alitangaza kumkaribisha waziri mkuu wa zamani Mh.Fredrick sumaye kwenye ulimwengu wa siasa za CHADEMA.

Swala hili hakika linazua maswali mengi sana.Ikumbukwe SUMAYE ni mmoja ya mafisadi papa wa nchi hii na alikuwemo kwenye LIST OF SHAME iliyosomwa na CHADEMA pale mwembe yanga.Je sumaye ameshakuwa msafi kiasi kwamba anapewa nafasi na CHADEMA?

Kelele za chadema siku zote ni kupingana na rushwa iweje leo mtuhumiwa mkubwa wa rushwa nchini kama sumaye aonekane muhimu mbele ya chadema na hatimaye kumtaka asajiliwe?

Lakini tuende mbali zaidi yawezekana MBOWE anamuita SUMAYE aje chadema kwa ile kauli ya WANYUMBANI NJOO NIKUSHIKE MKONO SIPO RADHI UFIE JANGWANI hatakama ni haramu??????.........ni siku chache sana SUMAYE amebwagwa kwenye uongozi ndani ya ccm na ameishia kulalama kuhusu kufanyiwa mchezo mchafu.

3. Kauli ya tatu tata zaidi ni ile aliyoitoa pale HAI alipokuwa anamkaribisha na kumshukuru Mh.Rais kikwete kwa utendaji wake.Mbowe alinukuliwa akisema"nimetembea angani na aridhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE."

Nachelea kusema maneno hayahaya yangesemwa na chama chochote kingine yangezua gumzo,au yange semwa na mwanachadema yeyote yule yangezua mjadala mkubwa wakitaifa.

Naomba kuuliza hii ni kauli sahihi ya kiongozi wa upinzani kumwambia Rais wa nchi hata kama ana show appriciation ya kile kilichofanyika?Hakuna lugha nyingine yakipinzani-yakusifia ambayoingetumika hapa???



Mbowe huu ni wakati wakuwekana wazi kwa watanzania, KAMA UKOMBOZI UMESHAUZWA NI HERI WATANZANIA WAKAAMBIWA kuliko maneno kama haya ya kusifia kupitiliza as if nchi hii hakuna upinzani.
WANA-JF nawasilisha naomba tujadiliane kwa makini namna kauli hizi zinavyoathiri chama na zinavyojenga chama.